0

Ajali hiyo ilitokea mwendo wa saa kumi na mbili asubuhi hii leo.
Boti moja iliyokuwa imebeba abiria 23 imegongana na mtumbwi wa wavuvi na kuzama katika ziwa Victoria Magharibi mwa Kenya.
Taarifa za awali zilikuwa zimetoa idadi hiyo kuwa 200 lakini maafisa wa usalama nchini Kenya wamethibitisha kuwa idadi ya abiria kwenye boti hiyo ilikuwa 23.
Watu 21 wameokolewa.
Miili ya watoto wawili imepatikana ikielea kwenye ziwa hilo.
Afisa huyo ameiambia BBC kuwa waliwaokoa watu 14 walipowasili katika eneo la tukio kabla ya kuwanusuru wengine saba waliporejea mara ya pili.
Wavuvi wanne waliokuwa kwenye mtumbwi wa pili pia waliokolewa.
Kwa mujibu wa walionusurika, boti hilo lililokuwa limewabeba abiria liligonga mtumbwi wa wavuvi kisha zote mbili zikazama majini.
Ajali hiyo ilitokea mwendo wa saa kumi na mbili asubuhi hii leo.
Ajali hiyo imetokea karibu na visiwa viwili vidogo ndani ya ziwa Victoria viitwavyo Kiwa na Remba Magharibi mwa Kenya.
Boti hiyo iliyokuwa na abiria ilikuwa inaelekea Sori kutoka kisiwa cha Remba.
Shughuli za uokoaji zinaendelea huku maafisa wa idara za serikali ya Kenya na wavuvi wakishirikiana kuwanusuru abiria hao.

Post a Comment Blogger

 
Top