0
Akiwa na umri wa miaka kumi na nane, mwanafunzi mmoja wa shule ya sekondari Mzumbe alishika mkononi gazeti la THE STANDARD[DAILY NEWS, kwa sasa katika maktaba na aliona tangazo lilikuwa linatafuta mtu atakayebuni jina la nchi inayoundwa na nchi mbili za TANGANYIKA na ZANZIBAR, kijana huyu mzaliwa wa Tanga aliamua kulifanyia kazi tangazo hilo ambapo alichukua herufi TAN kutoka neno TANGANYIKA, na herufi ZAN kutoka neno ZANZIBAR, hakuishia hapo, kutokana na uzoefu wake kuwa nchi nyingi za kiafrika ziliishia na herufi za IA, kama vile ETHIOPIA,GAMBIA,TUNISIA,NIGERIA,ALGERIA,SOMALIA,ZAMBIA na NAMBIA,aliona ni vyema basi azitumie herufi za IA ilikupa jina zuri ndipo neno TANZANIA lilipopatikana na kijana yule alituma jina hilo kwenda mamlaka husika.Mohammed Iqbal Dar aliibuka mshindi na alizawadiwa NGAO MAALUMU NA TSH 200. Kwa sasa Bwana Mohammed Iqbal Dar anaishi nchini Uingereza akifanya kazi ya uhandisi wa masuala ya redio. Mohammed Iqbal alizaliwa mwaka 1944 jijini Tanga

Post a Comment Blogger

 
Top