0
Davido na Diamond wakiwa pamoja mastaa wengine jijini Durban ambako kunafanyika tuzo za MTV MAMA

Hiyo ndio ilikuwa video ya kwanza ya Diamond kuifanya nchini Afrika Kusini ambapo aliwachukua Ogopa Videos kwa kazi hiyo. Kipindi hicho Diamond alikuwa ana uhusiano na Penny Mwingilwa. Miongoni mwa vitu alivyovifanya siku hiyo ni pamoja na kumfanyia surprise ya nguvu marehemu Mzee Muhidin Maalim Gurumo kwa kumzawadia gari.

Ulikuwa ni uzinduzi wa aina yake, uliofana na kwa kila mtu aliyekuwepo ilikuwa rahisi kuona ishara ya mafanikio makubwa yaliyokuwa mbele ya mtoto huyu wa Tandale.

Mambo yalikuja kubadilika zaidi October 2013 baada ya Davido kuja Tanzania kwenye Fiesta ya Dar es Salaam. Mazungumzo yalifanyika na Davido kukubalika kuibariki remix ya Number One.

Wawili hao walifanya video ya remix hiyo nchini Nigeria chini ya muongozaji Clarence Peters. Baada ya video kutoka, mambo hayakuwa kama zamani tena. Kipindi hicho Davido alikuwa msanii hot sana Afrika na hivyo kwa Diamond kumpata kwenye remix yake kilikuwa ni kitu sahihi alichowahi kukifanya katika maisha yake.

Kabla ya hapo jina la Diamond lilikuwa ni kubwa tayari Afrika Mashariki, lakini si Magharibi. Remix hiyo ikapendwa, audio na video vikaanza kupata airtime kwenye redio za Nigeria, Ghana na Afrika Kusini. Davido akasaidia kumweka kwenye ramani Naseeb Abdul.

Haichukua muda, nominations zikaanza kumiminika. BET Awards, MTV MAMA hadi CHOAMVA. June 2014, Diamond akapata bahati kutumbuiza kwa mara ya kwanza kwenye jukwaa la tuzo hizo jijini Durban, SA akiwa na Davido.

Kadri muda ulivyokuwa ukienda, Diamond akaanza kuwa mpinzani wa Davido kwenye tuzo nyingi na ‘tension’ ikaanza kuzaliwa. November 29, Diamond akaibuka mshindi wa tuzo tatu kwenye CHOAMVA na kuwa mbele ya Davido ambaye wengi walihisi hakufurahia.

December 2014, kwenye fainali ya Big Brother Africa, ‘bifu’ ikazaliwa. Ushindi wa Idris Sultan ukamfanya Davido atweet ujumbe uliowakasirisha watanzania wengi. ‘And they cheat again.’

Usiku huo huo Diamond akashinda tuzo zingine zilizokuwa zikitolewa jijini Lagos na akajibu dongo la Davido. Kauli ya Davido ikamweka kwenye kitimoto na kuambulia matusi mengi hadi kutukaniwa mama yake. Bifu ikawa kubwa. Duru za chini ya kapeti zikadai kuwa kambi ya Davido ikatangaza vita kwa Diamond. ‘Speculations’ za bifu yao ziliendelea kwa muda mrefu licha ya mameneja wa Diamond, Babu Tale na Salaam kukanusha mara kadhaa kuwa hakuna bifu kati yao.

Nominations za MTV MAMA 2015 zikawarudisha tena wawili hao kwenye ‘tension.’ Katika muda ambao uadui wa Team Diamond vs Team Kiba ulikuwa umepamba moto, Diamond na Davido wakajikuta wakilazimishwa kutoolewana na hadi July 15, 2015 bado wengi tuliamini kuwa Diamond na Davido haziivi.

Picha zilizowekwa jana kwenye Instagram zinazowaonesha Diamond na Davido wakicheka kama vile hakuna kilichowahi kutokea, zimepokelewa kwa furaha kubwa na mashabiki wao.

Source:udakuspe..

Post a Comment Blogger

 
Top