0
Tofauti kati ya Mrema na Lowasa wote wakiwa wametokea CCM na wote wakiwa wagombea uraisi kupitia upinzani walikoingia bila kujua sera za vyama walivyoingia kwa kuwa waliingia chap chap ni kama ifuatavyo

1.Mrema alikuwa akiungwa na makundi ya wasomi waliobobea wakiwemo maprofesa walikuwa tayari kumbeba na kusukuma gari lake kuonyesha upendo wao kwake.Lowasa wasomi wamekaa naye mbali wengi hata kumsikia hawataki kuanzia wasomi wakubwa hadi wadogo.Slaa alikuwa kipenzi cha wasomi

2.Mrema aliungwa na watu wengi wa hali ya chini (walalahoi) ambao walimpenda bure bila gharama yeyote kwa kuwa alijitambulisha kama mlalahoi mwenzao wakawa wanamwunga mkono na kumsindikiza kwa makundi makubwa ya kutisha wakihemka kwa mihemko ya dhati ya kumwunga mkono mgombea wao.Lowasa haungwi mkono na walalahi wengi kwa kuwa kajitanabaisha kama mtu mwenye pesa anayetaka kumkomboa mlalahoi!! Walalahoi wazo la kukubali kuwa tajiri aweza kuwakomboa wengi wanalikataa hivyo Lowasa kumfanya akose waunga mkono kutoka kundi la walalahoi.Walalahoi wengine ambao wako tayari kumfuata ni wale ambao wanaamini kuwa Lowasa ana hela na wanataka pesa zake kwanza ili waandamane naye ana WAFUASI MASLAHI WENGI MNO ambao hawamwungi mkono kwa dhati kama ilivyokuwa kwa mrema.

3.Mrema alipoondoka CCM aliondoka na wafanyabiashara wengi wazawa kibao ambao walikuwa wakinyionyesha wazi na kumchangia hasa kwa ajili ya mbio za uraisi bila woga na kwa mapenzi ya dhati kwa mrema.Lowasa anaoondoka nao CCM ni watu maslahi si watu wenye hela wanaotaka kumsaidia bali wengi ni wale omba omba wavizia pesa za Lowasa wanaosubiri Lowasa atafute pesa awagawie!! Ziwasaidie ubunge,udiwani au katika mishe mishe za maisha yao.Ni watu wenye tamaa ambao wangependa wapenye waingie ndani ya Team lowasa kule kwenye fuko la hela hasa walibomoe.
Makundi ya wengi wanaohama CCM kumshabikia Lowasa ni wachovu kipesa na kimaisha wamepigika.Wanavizia LOWASA

4.Mrema alibebwa na vyombo vya habari bure hakutoa hata thumuni na misafara ya wasindikizaji ilikuwa ni ya bure hakuwapa chochote.Lowasa kuanzia vyombo vya habari visivyokuwa na haya kutwa vinawinda hela yake na wasindikizaji kuanzia bodaboda wanasema HAPENDWI MTU NI POCHI TU alete pochi tuingie barabarani.

5.Mrema alijipambanua kama mpiganaji wa wazi wa ufisadi Lowasa kauli mbio yake ni ya kuondoa CCM ,ufisadi ulimi wake unashindwa hata kutamka

Kwa ujumla Mrema alikuwa na nguvu kubwa kuliko Lowasa ya uungwaji mkono wa dhati.Kwa kuangalia aina ya waunga mkono Lowasa sisiti kusema uwezo wake wa kushinda Uraisi ni mdogo mno.Angekuwa na Sifa za mrema angalau angefurukuta.

Maoni Binafsi Kutoka Kwa YEHODAYA -JF

Post a Comment Blogger

 
Top