0
Mgombea urais kupitia chama cha mapinduzi CCM Dokta John Magufuli amesema wanachama wa chama hicho hawana haja tena ya kutofautiana kauli baada ya hatua za kuwapata wagombe wa kupeperusha bendera za chama hicho kukamilika.
Dokta Magufuli amesema hatua iliyo mbele ya chama hicho kwa sasa ni kufanya kampeni zenye tija katika harakati za kuhakikisha CCM inaendelea kuwa chama tawala nchini.
 Kukutana na wazee na wanachama wa chama cha mapinduzi mkoa wa Dar es salaam ni tamaduni iliyojengeka miaka mingi ambayo inaaminika kundi hilo hutoa busara kwa kiongozi wanayekutana naye.Hii ni mara ya kwanza kwa Dk.Magufuli kupata fursa ya kukutana na wazee hao kunadi uwezo wake.
Ambapo Muhamed mtulia mwenyekiti wa wazee mkoa wa Dar es salaam pamoja na kufanyika kwa kikao hicho ameshauri kufanyika kwa kikao kingine rasmi ili kumuelekeza mengi yanayoihusu Tanzania.

Post a Comment Blogger

 
Top