0
Makanisa yaliyochomwa moto ni Pentecostal Assembilie of God (PAG) kata bakoba eneo la buyekera,Living Water International na Evangelical Assemblies of God (EAGT) kata ya Kibeta yote ya mjini Bukoba .Chanzo chake hakijafahamika ambapo wachungaji na viongozi wa kiroho wanaomba vyombo vya dola kuwabaini wahusika.

kamanda wa polisi mkoani kagera Augstine Oromi amedhibtisha kutokea kwa tukio hilo na amemweleza mwandishi wa mtandao huu kuwa yupo katika ziara ya kazi wilayani ngara hivyo atatoa taarifa baadaye.

Matukio ya makanisa kuchomwa yameshamiri katika manispaa ya bukoba ambapo hili ni tukio la sita kwa kipindi cha mwaka mmoja

Post a Comment Blogger

 
Top