0
“Kwa hiyo akinikuta saa hizi humu ndani
kwake si ataniua?”

Hawezi, ingawa ana bastola…”
“Mama mimi nakwenda, kumbe mumeo ana
bastola..!”
“Hawezi kukuua, alisema hataki uingie usiku,
‘asa kwani saa hizi ni usiku?”
alisema mama Joy huku akimsogelea mzoa taka huyo
na kumshikashika kidevuni. Alizikuna ndevu zake chache…
“Una ooo nzuri kijana, sema tu hutaki
kuitunza…”
“Una macho mazuri, madogoooo, sema tu
unayashindisha juani mpaka yanakuwa mekundu, au unavuta bangi..?”
“Sivuti bangi mama…”
 
“Una midomo mizuri, minene halafu myeusi,
naipenda.” Hapo mama Joy vidole vyake vilikuwa vikicheza kwenye midomo ya mzoa
taka huyo ambaye alionekana hajapiga mswaki…
“Halafu kifua chako kimetuna vizuri sana, mi
nakipenda, unafanyaga mazoezi  nini?”
“Nina muda huo mama, labda kimetuna chenyewe
tu.”
 
Mama Joy alimvutia kwake mzoa take,
akamgusanisha na kifua chake huku akizidi kummwagia sifa kibao…
“Halafu kifua chako kina joto zuri…”
“Asante mama…”

“Halafu masikio yako yamekaa vizuri kwa
kushikwashikwa,” mama Joy akamshika masikio mzoa taka huyo…
“Mama unanitekenya lakini…”
“Kweli..?”
“Kweli tena…”
 
“Nakutekenya nikifanyaje?”
“Hivyo unavyonishikashika masikio…”
“Yaani hivi,” alisema mama Joy akiendelea
kumshikashika sehemu hizo, mzoa taka akachachamaa mwili, akatupa furushi lake
chini.
 
Kutokana na maisha yake ya kifukara ambapo
kula, kulala kwake  kwa kubahatisha, mzoa
taka hakuwa akipata mademu, kwa hiyo mama Joy kumfanyia ‘utani’ ule wa kimahaba
kwake ilikuwa kama mtende ulioota kwenye jangwa…
 
“Unajua mwenzio naumia mama, kwani nini
kimetokea mpaka leo unafanya hivi..?”
“Kijana tulia, kwani siku zote hukuona kama
nimekupenda sana mwenzio..?”
“Aaah! Mama wewe mke wa mtu, mimi siwezi,
naogopa na sitaki.”
 
Mama Joy alijua kauli ya mzoa taka huyo ya
kugoma inaweza kuzua matatizo makubwa kwamba atamtangaza, akaamua kumbaka.
Kwanza, aliangalia kulia na kushoto,
alipoona hakuna mtu na mlinzi hawezi kufika, alimshika mzoa taka na kumlaza
chini kwenye nyasi za bustani, akamvua suruali, akamvua ‘kufuli’ kisha yeye
akavua zake na kuanza kujihudumia kwa raha zake…
“Mama…”
“Abee…”
“Mumeo ana bastola lakini…”
“Wala isikutishe, ha…ha…wezi kuja…”
“Akija je?”
 
“Ni…nisi…kie mi…mi…”
Kwa kuwa walikuwa wanaiba, mama Joy
alijitahidi kupiga mashuti ya kasi ili apate goli la ushindi. Hakukuwa na
mbwembwe, madoido wala manjonjo, mama Joy akafika juu ya mlima na kutangaza
ushindi.
 
Aliamka na kumsimamisha mzoa taka ambaye
bado alikuwa hoi kwa ‘mzuka’ ingawa naye alishabanjua dafu lake moja, lakini
bado alikuwa anataka tena…
“Simama basi.”
Mzoa taka alisimama…
“Vaa…”
Mzoa taka alivaa nguo zake, akaendelea
kusimama…
 
“Chukua matakataka yako, mimi nakuja sasa
hivi,” alisema mama Joy huku akienda ndani.
Mzoa taka alijishangaa kwa jinsi alivyobaki
na harufu ya pafyumu ya mama Joy…
“Mmm…ananukia vizuri, sijui kajimwagia nini
mwilini?”
 
Baada ya dakika mbili tu, mama Joy alirudi,
akampa mzoa taka shilingi elfu hamsini, nyekundu tupu…
“Hizi ukanunue suruali nzuri, shati zuri,
viatu, chup* na kisha uoge uwe mzuri zaidi ya hapa, sawa kijana wangu?”
 
“Asante sana mama, sawa.”
Mzoa taka aliweka pesa mfukoni, akabeba
furushi lake na kutoka.
Getini, mlinzi alimtupia jicho baya mzoa
taka…
 
“Hivi wewe kijana, huko mitaani hakuna
matakataka hadi uje hapa?”
“Sasa kwani yako?”
“Jibu swali wewe, acha ujeuri, nitakuwa
sikufungulii…”
 
“Usifungue tuone kama nitakuwa siingii…”
“Utaingia kwa njia gani?”
“Pana nini hapo getini..?” mama Joy aliuliza
kutokea mbali karibu na mlango mkubwa wa kuingilia ndani…
“Si huyu hapa,” alisema mzoa taka…
“Anasemaje?”
 
“Mama namtania tu huyu ni mtani wangu. Teh!
Teeh! Teeeh!”
Mama Joy aliingia ndani. Mwili wote ulikuwa
ukinuka jasho la mzoa taka. Mbaya zaidi alimchafua hadi  nguo aliyovaa…
“Daaah! Yataka moyo kuwa na mpenzi kama
huyu,” alisema moyoni mama Joy, mara honi ya gari mlangoni ikalia…

“Mh! Siyo mume wangu kweli huyo?”
“Na kama ni mume wangu si ajabu amemuona
mzoa taka,” aliwaza mama Joy huku akikimbilia chumbani, akachukua taulo kisha
akakimbilia bafuni ambako alioga kwanza.
Alipotoka alimkuta mumewe amekaa sebuleni.
Mama Joy alitetemeka sana…
“Vi…pi mwenzetu?”
 
Baba Joy alimkazia macho mkewe bila kumjibu
kitu halafu akaangalia kwenye tivii ambayo ilikuwa haijawashwa…
“Baba Joy.”
Baba Joy alimwangalia mkewe kama ishara ya
‘nakusikiliza ongea’. Lakini mama Joy alipoona hali ile, hakuongeza neno,
alipitiliza chumbani…
 
“Mh! Hapa kuna ishu, lazima.”
Licha ya kujikausha kwa taulo lakini
aliendelea kuhisi ananuka uchafu aliogusishwa na mzoa taka. Alivaa gauni simpo,
akatoka hadi mlango mkubwa, akatumbukiza miguu kwenye sendozi, akaelekea
getini…
“Mlinzi…”
 
“Naam mama…”
“Baba Joy alipoingia alisemaje?”
“Hajasema kitu, amepiga honi tu kisha
akaingia.”
“Ulimwamkia?”
“Ndiyo mama.”
“Akaitikiaje?”
 
“Kha! Mama kwani wewe nikikuamkiaga huwa
unaniitikiaje?”
“We mshe
nini? Nakuuliza swali na wewe
unanijibu swali…”
“Alisema marhaba, nikamuuliza mbona umewahi
kurudi? Akasema amechoka sana…”
 
“Mlinzi fungua geti haraka,” sauti ya baba
Joy ilisikika kwa kishindo na vile ilikuwa nzito na nene ndiyo kabisa.
Baba Joy aliingia kwenye gari, likarudi
‘rivasi’ na kugeuza kisha likatoka ndani bila kuaga mtu. Mlinzi alifunga geti
nyuma ya baba Joy…
“Mlinzi,” mama Joy aliita…
 
“Naam mama…”
“Hebu njoo huku ndani,” mama Joy alisema
huku akianza kutembea. Alipofika sebuleni, alikaa mkao wa hasira.
Mlinzi aliingia…
 
“Nifunge mlango mama..?”
“Wa nini..?”
“Nilikuwa nauliza tu…”
“Hebu kaa hapo.”
Mlinzi naye alianza kutetemeka, alihisi
kibarua kimeingia mdudu mbaya…
“We mlinzi si una namba ya mume wangu..?”
“Ndiyo…”
“Simu yako iko wapi?”

JE NINI KITAENDELEA ...USIKOSE...SEHEMU YA ....03... 

Post a Comment Blogger

 
Top