0
Mamlaka ya chakula na dawa kanda ya kaskazini kwa kushirikiana na jeshi la polisi wamembaini na kufanikiwa kumkamata mfanyabiashara mmoja jijini Arusha anayemiliki kiwanda bubu kinachotengeneza vipodozi bila usajili wa TFDA pamoja na shehena ya zaidi ya tani saba ya vipodozi mbalimbali vikiwemo vile vilivyopigwa marufuku vikiwa vimehifadhiwa kwenye ghala lisilokidhi viwango
Akizungumza na Ripota wetu katika eneo la tukio mtaa wa Sakina mkuu wa operesheni wa TFDA Benson Mcheza anasema wamefanikisha zoezi hilo baada ya kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema na kwamba mtuhumiwa atachukuliwa hatua za kisheria na kulipia gharama zote za kuteketeza bidhaa hizo
Kwa upande wake mfanyabiashara anayemiliki kiwanda hicho Chalo Makala amesema bidhaa zilizoko kwenye ghala ni bidhaa za dukani kwake ambazo amelipia kodi zote stahiki na kwamba zile anazozalisha zilikua kwenye majaribio.
Kwa upande wa uongozi wa kata ya Kiranyi kilipo kiwanda hicho wakatoa wito kwa jamii kutoa taarifa mapema pale wanapobaini uendeshaji wa biashara yoyote kinyume cha sheria ili kuepusha madhara kwa watumiaji lakini pia kuziba mianya ya ukwepaji kodi.

Post a Comment Blogger

 
Top