0
Mh mbunge wa Arusha mjini amegoma kula tangu amewekaa maabus zinaendelea kusambaa kwa kasi,hiii ni baada ya maelezo yaliyotolewa na meya wa jiji la arusha bwana Calist Lazaro ambapo amesema Mh.Lema amelazimika kugoma kula baada yakutoridhika na ukamatwaji wake ambao ameutafsiri kama udhalilishwaji mbele ya familia yake.

Nalazimika kusema madai ya muheshimiwa mbunge Kugoma kula niyamsingi ila ameyafanya kwa kukurupuka,kiasi chakukosa mashiko,haswa kwa wanaomshikilia, mh lema Hajatuambia ni nini hasa anataka afanyiwe ili arejee kula kama kawaida,alipaswa kuliambia Jeshi la Polisi kama walimkamata kwakumdhalilisha mbele ya familia yake,basi polisi Wakaombe radhi kwa familia na watoto wake ndio arejeshe hali yake ya kula kama kawaida,

Niwazi watu wote wanaotumia njia hii kudai haki huweka masharti ambayo yakitekelezwa hurejea kula kama kawaida,mh Mbunge hoja yake ya msingi lakini ameishia kusema amegoma kula Kwa sababu amekamatwa kwakudhalilishwa mbele ya familia yake,ingependeza kama angeenda mbali zaidi kuliambia Jeshi la Polisi lifanye jambo gani ili arejee kula kama kawaida.

Baada ya kusema hayo naomba nimpe pole za dhati mh lema,sote tunafahamu maabusu sio pazuri Mh LISU alikaaa siku moja akatupa ushuhuda MAABUSU sio pazuri,LEMA umekaa siku Tatu tunakila sababu kukupa Pole.

Nawasilisha

Post a Comment Blogger

 
Top