0
Walimu 22 wa Shule ya Sekondari ya Azania Manispaa ya Ilala, akiwamo Mwalimu Mkuu, wamehamishwa kwa kile kilichodaiwa ni kutokana na matokeo mabaya ya kidato cha sita.

Chanzo hicho cha habari kiliongeza kuwa kati ya walimu hao, 17 walikuwa wanafundisha kidato cha tano na sita huku wanne kidato cha kwanza hadi cha nne na mmoja aliyekuwa mkuu wa shule hiyo.

Taarifa hizo ziliongeza kuwa kati ya walimu 17, wengi wao walikuwa wanafundisha mchepuo wa ECA ambao wote wamehamishwa na kupangiwa shule nyingine huku wengine wakihamishiwa shule za kata na kupangiwa kufundisha kidato cha kwanza, pili na tatu. Awali, walimu hao walikuwa wakifundisha kidato cha tano na sita.

Hivi karibuni Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), lilitangaza matokeo ya kidato cha sita na shule hiyo kongwe ikajikuta imo katika kundi la shule 10 za mwisho zilizokuwa na matokeo mabaya.

Post a Comment Blogger

 
Top