0
Rapper Desiigner ambaye anafanya vizuri duniani kote na rekodi yake ya PANDA amekamatwa na polisi kwa kosa la kukutwa na silaha na dawa za kulevya kwa mujibu mtandao wa TMZ.
desiigner
Polisi imesema Desiigner na watu wengine wanne walikuwa kwenye gari waligombana na dereva mwingine ambaye alipiga simu polisi kuripoti tukio hilo.
Na baada ya polisi kusimamisha gari alilo kuwepo Desiigner walikuta dawa kama OxyContin na kuwakamata vijana wengine wanne.
Desiigner amefunguliwa mashtaka ya kukutwa na dawa za kulevya akiwa na nia ya kuuza pamoja na watu wengine wanne, kosa la kutembea na silaha yenye risasi na kosa la kutishia. kuna kampeni ambayo inaitwa #FreeDesiigner imetumika kama kampeni ya kumtoa jela.

Post a Comment Blogger

 
Top