0

Mabingwa wa ligi ya soka nchini Kenya Gor Mahia walitoka nyuma na kuinyamazisha timu ya yanga kutoka Tanzania 2-1 katika mechi yao ya ufunguzi wa kombe la CECAFA katika uwanja wa kitaifa wa Dar es Salaam.
K'Ogalo kama wanavyojulikana walikabili tishio la Yanga baada ya beki Dirkir Clay kujifunga mwenyewe na kuweza kufunga mabao mawili kupitia Harun Shakava na mshambuliaji Michael Olunga katika mechi ya kusisimua ambapo Yanga ilimaliza ikiwa na wachezaji 10 uwanjani.
Shakava alifunga bao la kusawazisha baada ya kufunga kichwa kizuri kutoka kwa mkwaju wa adhabu uliopigwa na Karim Nizigiyimana baada ya Godfrey Walusimbi kuangushwa upande wa kushoto kunako dakika ya 18 kabla ya Olunga kuimarisha mambo na kuiweka Gor kifua mbele dakika moja baada ya kipindi cha mapumziko.
Nahodha wa timu ya Yanga Nadur alikosa penalti katika kipindi cha pili baada ya Shakava wa Gor Mahia kuunawa mpira katika eneo la hatari huku kipa wa Gor Mahia akiudaka mkwaju wake kwa urahisi.
Katika mechi nyingine ya ufunguzi, KMKM ya Zanzibar waliwafunga Telecom ya Djibouti 1-0 katika uwanja wa kumbukumbu ya Karume.
APR ya Rwanda pia iliwafunga Al-Shandy ya Sudan 1-0 katika mechi iliyoanza kabla ya ile ya Yanga vs Gor Mahia katika uwanja wa Taifa.
Sehemu ya ratiba ya michuano hiyo inayodhaminiwa na Raisi wa Rwanda, Paul Kagame ni kama ifuatavyo:

Post a Comment Blogger

 
Top