
Machemli, aliyekuwa Mbunge wa Ukerewe mkoani Mwanza, alijikuta akishindwa kupata kura za kutosha katika uchaguzi huo uliofanyika juzi mjini Nansio, Ukerewe.
Awali, uongozi wa Chadema Makao Makuu ulikuwa na mapendekezo kwamba wabunge wa majimbo wa chama hicho wapite bila kupingwa na ingawa wengi walikuwa na wapinzani, wamefanikiwa kuvuka kizingizi cha kura za maoni isipokuwa Machemli.
Aliyembwaga Machemli ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Joseph Mkundi, aliyepata kura 232 kati ya 466 zilizopigwa, akiwashinda wagombea wengine tisa huku Machemli akiambulia kura 74.
Post a Comment Blogger Facebook