 MBUNGE  anayemaliza muda wake, Salvatory Machemli, amekuwa Mbunge wa kwanza wa  jimbo kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kubwagwa kwenye  kura za maoni zinazoendelea ndani ya chama hicho.
MBUNGE  anayemaliza muda wake, Salvatory Machemli, amekuwa Mbunge wa kwanza wa  jimbo kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kubwagwa kwenye  kura za maoni zinazoendelea ndani ya chama hicho.Machemli,  aliyekuwa Mbunge wa Ukerewe mkoani Mwanza, alijikuta akishindwa kupata  kura za kutosha katika uchaguzi huo uliofanyika juzi mjini Nansio,  Ukerewe.
Awali,  uongozi wa Chadema Makao Makuu ulikuwa na mapendekezo kwamba wabunge wa  majimbo wa chama hicho wapite bila kupingwa na ingawa wengi walikuwa na  wapinzani, wamefanikiwa kuvuka kizingizi cha kura za maoni isipokuwa  Machemli.
Aliyembwaga  Machemli ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Joseph Mkundi,  aliyepata kura 232 kati ya 466 zilizopigwa, akiwashinda wagombea wengine  tisa huku Machemli akiambulia kura 74.
 
Post a Comment Blogger Facebook