0
Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Damian Lubuva .

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa imeongeza muda wa siku nne wa kuandikisha wapiga kura kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam. Hii inamaanisha kuwa zoezi hilo ambalo lilikuwa linaisha leo ijumaa ya julai 31, litaendelea hadi jumanne agosti 4.
Akiongea na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa NEC, Jaji Mstaafu Damian Lubuva amesema kuwa hataweza kuongeza muda wa zaidi ya siku nne kwa kuwa ratiba zitaingiliana.

Aidha, Jaji Mstaafu Lubuva amesema mpaka sasa watu zaidi ya milioni 18 wameandikishwa katika daftari la kudumu la wapiga kura kwa njia ya mfumo wa kielektroniki BVR kwa nchi nzima.

Post a Comment Blogger

 
Top