0
1. Yamoto Band wameshangiliwa zaidi kuliko Magufuli

2. Wakati Mbowe amewakutanisha Lowasa na Sumaye. Leo Jakaya amewakutanisha Diamond na Ali Kiba Jangwani,

3. CCM wanajua kuwa mikutano ya UKAWA inapata mafuriko, kwa hiyo nao walijitahidi wapate "mafuriko"

4. Watu wengi wameenda kuwashangaa wasanii, sio kumsikiliza Magufuli. Kumuona Diamond bei ghali, leo wamemuona Live bila kiingilio wataacha kwenda?

5. Magufuli anajua lugha nyingi za makabila kuliko anavyojua matatizo ya wananchi,

6. Mkapa anahitaji maombi ya kufunga maana anazeeka vibaya. Amemuita Mpumbavu, Waziri Mkuu aliyemteua mwenyewe na kufanya nae kazi miaka 10,

7. Mwisho wa mikutano ya siasa ni saa 12 kamili lakini CCM wamezidisha dakika hadi 12:40. Ikiwa wameshindwa kutekeleza Sheria waliyoiweka mwenyewe, watawezaje kutekeleza ahadi zao? CCM hawapaswi kuaminiwa,

8. Kitendo cha Magufuli kukiri serikali inanyanyasa Machinga na mama Ntilie ni kukiri kuwa serikali yake imechoka na inahitaji kubadilishwa,

9. Magufuli amemvua nguo Kikwete hadharani. Kusema anashangaa meno ya tembo yamefikaje uarabuni ni kusema kuwa JK anashiriki biashara hiyo. Ikiwa Magufuli amesema atazuia biashara hiyo haramu, nini kimemshinda JK kuzuia kwa sasa?

10. Magufuli anajua kuwa CCM inakaribia kufa. Wakati akimalizia hotuba yake ametoa mfano ambao haukueleweka vizuri, lakini fundisho lake ni kuwa WATANZANIA MSIIUE CCM. Kumbe anajua kuwa CCM itakufa,

11. Ccm wamewadharau sana watanzania kwa kuwapandisha malori ya kubebea vitunguu, nyanya na viazi. Mtanzania aliyepandishwa lori leo akiipigia kura CCM atadhihirisha kuwa yeye ni kiazi,

12. Mzee Warioba ameshindwa kabisa kumnadi Magufuli kwa hoja. Kwa namna alivyojieleza anaweza kuzidiwa na kijana aliyemaliza form four akapata division zero,

13. Mzee Mkapa ana matusi "makali" kuliko wafanyakazi wa bar,

14. Bila msaada wa malori na kujazia bodaboda mafuta, uwanja wa Jangwani leo ungekua mtupu,

15. Warioba anaipenda CCM zaidi ya anavyoipenda Tanzania,

16. Rais Kikwete amekiri kuwa Magufuli alikua chaguo lake, it means hakuwa chaguo la wanaCCM. Kwa lugha rahisi Kikwete amedhihirisha kuwa alienda Dodoma akiwa na majina yake mfukoni kama ilivyodaiwa,

17. Kwa kuwa Polepole alikiri Warioba ni "Role Model" wake, leo tumemjua anayemtuma Polepole kutukana UKAWA,

18. Jeshi la Polisi linatumika kisiasa. Wameshindwa kuzuia maandamano "haramu" ya CCM na kuzuia mkutano ilipofika saa 12 kamili kama sheria inavyotaka,

19. Miongoni mwa watu wanaopaswa kuchunguzwa UKAWA ikishika dola ni pamoja na Jaji Joseph Warioba na Mzee Mkapa,

20. CCM haifai kuendelea kuwa madarakani baada ya October 25

Post a Comment Blogger

 
Top