0
YAMOTO

Ni Uzinduzi wa Video ya Cheza kwa Madoido...  


KUNDI linalotikisa kila kona la Yamoto Band linatarajiwa kuzindua staili mpya za kucheza, Septemba 11, mwaka huu pale watakapozindua rasmi Video ya Cheza kwa Madoido ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live uliopo Mbagala-Zakhem jijini Dar.
Akichonga na Mikito Nusunusu, meneja wa bendi hiyo, Said Fella aliwataka mashabiki wa Yamoto kufika kwa wingi kutokana na staili walizoandaliwa na kuongeza kuwa usiku huo utafunikwa na ‘sapraizi’ kibao kutoka Mkubwa na Wanawe wakiongozwa na Chegge na Temba.
“Kama ilivyo Video ya Cheza kwa Madoido ndivyo itakavyokuwa kwa laivu jukwaani kwani usiku huo utakuwa wa aina yake. Tunatarajia pia kuwa na sapraizi ya kimataifa,” alisema Fella.
Video hiyo imepikwa nchini Sauz chini ya Kampuni ya The Godfather.

Post a Comment Blogger

 
Top