0

Yemi Alade, Ycee, Cassper Nyovest na Alikiba wanatarajiwa kuwasha moto kwa kutumbuiza kwenye kilele cha tuzo za MTV MAMA 2016.

Tuzo hizo zitafanyika October 22, 2016, kwenye ukumbi wa Ticket Pro Dome, Johannesburg, Afrika Kusini.

Rapper wa Afrika Kusini, Nasty C na muimbaji wa nchi hiyo, Babes Wodumo nao watatumbuiza. Majina ya wasanii watakaowania tuzo hizo mwaka huu yatatajwa, jijini Johannesburg mwezi huu.

Post a Comment Blogger

 
Top