0
Mkurugenzi wa Mkubwa na Wanawe Foundation na Yamoto Band, Mkubwa Fela amewataka mashabiki wa muziki kusubiria mambo makubwa kutoka katika brand ya Yamoto Band huku akiwata mashabiki hao kuchangamkia nguo mpya za brand hiyo ambazo zimeingia sokoni hivi karibuni.
ymoto
Akiongea na Bongo5 wiki hii, Mkubwa Fela amesema nguo za brand ya Yamoto Band tayari zimeingia sokoni za zinapatikana katika maduka mbalimbali.
“Kuna mambo mengi yanakuja, tuombe uzima lakini kwa sasa tunazungumzia mzigo mpya ambao umeingia sokoni, nguo ni nzuri tunahitaji support za mashabiki wetu katika kutuungisha,” alisema Fela. Kwa sasa mzigo upo umeingia sokoni na unapatikana katika maduka mbalimbali,”
Pia Fela amesema tayari ameshasajili logo ya brand ya Yamoto Band ili kukabilina na watu ambao watajaribu kutengeneza bidhaa feki.

Post a Comment Blogger

 
Top