0
Akihojiwa na mtangazaji wa AZAM TV wakati wa taarifa ya habari ya saa 2 usiku leo katibu wa CUF Tanzania bara Magdalena Sakaya amekiri kuwa CUF hawamo kwenye kikao cha UKAWA kinachoendelea jijini Dar es salaam

Katika ufafanuzi wake amesema CUF wametoka kwanza wajadiliane maoni waliyoyapokea kutoka kwa wanachama wao wakiafikiana watarudi na kujiunga na UKAWA

Hayo yanatokea wakati tunaambiwa muda wowote UKAWA watamtangaza mgombea na kutoa nini wamekubaliana. Tusubiri tuone maana hali hiyo siyo njema na haitoi ishara njema kwa upinzani nchini

Post a Comment Blogger

 
Top